BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, May 17, 2010

'LYRICS YA MR PRESIDENT'- NGOMA YA ROMA


SONG MR-PRESIDENT
ARTIST R.O.M.A
PRODUCER J-RIDER + YUDDI
STUDIO TONGWE RECORDS
romabraq@yahoo.com


INTRO
By…..Mwl. Julius Kambarage Nyerere
Ikulu ni mahali patakatifu, ikulu ni mahala patakatifu,
Mimi sikucha guliwa na wananchi wa Tanzania
Kuja kupageuza kuwa pango la walanguzi
Claps claps claps
By…Roma
Drop drop drop drop drop yop
Haaa haaa… yes Surprise …Tongwe records
We are here for revolution wooord
Mr. president ..welcome to white house
Thank you….aaaah …thank you ….yeaaah

VERSE….1
Mi ndo’ roma mkatoliki mwenye asili ya kiyahudi
Mpare wa milimani sa lamu ya kikwetu urewedi
We ni mkwere wa chalinze ambaye hutamsahau mnyakyusa...(Mwakyembeee)
Aliye wafundisha monduli siasa
Aliyekula kiapo kwa agano jipya la wakorintho
Siyo msabato mwenye siasa za kubattle kama Zitto
Mwenye wito wa Appocalypto husssle za Kambikatoto
Msaka ndoto kama kristo shujaa kama Mrisho Mpoto
Jasiri kama Mandela busara kama Nyerere
Niliyejificha mapangoni mithili ya Otango Osale
So usinidanganye kwa uchawi waaa kutumia ndulele
Au vita vya majimaji nife kama Kinjekitile
Hatutaki siasa za kale, siku hizi tunawahi kubalehe
Nawapa pole wakazi wote wa Tandale kwa Mtogole
Akhsante Sheikh umeniita ikulu sio kisa nina nyota ya mshale
Najua mvi sio busara ila naomba amani itawale
Ikulu yako ina thamani zaidi ya falme za kiarabu
Cha ajabu hawaithamini na inapoteza thawabu
Taifa lilikutabri tangu enzi ukiwa waziri
J.K wa 2 utakuja ongoza hii serikali
Yenye vilio kote kama kina mama wa Galilaya
Wanaoutafuta ukombozi wasimamishe Pobilahaya
Viongozi wetu ni mafia na mabeautifull lier
Nilikuwa na ndoto hizo ila bado hawaja niinspire

CHORUS
Pagani si mlituahidi mtamwaga na lami vipiii?...Badoooo
Wanafuzi mlituahidi walimu mtawaleta!!...woooh
Morogoro na Tanga vipiii?Badooo
Dodoma…?Badooo…
Kigoma…?Badooo..
Maisha bora kwa watanzania nyie wenyewe mlituambia
Manurse…?Badooo
Mapolice…?Badooo
Ajira kwa vijana na maendeleo kwa kina mama
Watotoo…?Badooo
Kina mamaaa…?Badoooo

VERSE….2

Inafahamika ulipewa nchi angali imeshachafuka
Uongoze hii familia kubwa ya kizazi cha nyoka
Na ukakubali kubeba huu msalaba wa ukombozi
Hizi kashfa ndo’ changamoto zisikutoe machozi
Sitosahau campaign zako za mwaka 2005
Nilichomwa na jua nikingoja upite nipunge mkono
Traffic aliyepangwa saa moja kisha ukapita saa saba
Akiwa na stress za mwanae shuleni kafukuzwa ada
Leo mna nyumba mna mashamba mna viwanja mna viwanda
Mi nasaga na rhumba na mshahara wangu haujapanda
Yule traffic maisha magumu aaah muogopeni Mungu
Nikisema it is not fair mnataka mnifunge pingu
Gerezani kesi za wanyonge cheki zinapigwa tarehe
Jamhuri itafata mkondo ee mola wangu wasamehe
Wasaliti kama Eskarioti mbele ya Yesu Mnazarethi
Wa sakramenti ya ekaristi bado hawaitaki torati!!
Harakati ndo’ jadi siogopi hadi wanichape mjeledi
Hadi yuddi alikuwa shahidi kwa vinanda na vinubi
Elimu yetu bahati nasibu kama mikopo ya desi
Kimbilio la waliofeli ni ualimu na upolisi
Wamefisadi tenda ya rada, ndege ya raisi, magari ya jeshi
Wote matraitor sasa skrepa kama Lubumbashi
Wanapata alama za juu kwa kumuhonga penzi professor
Mtunza pesa wa benki kuu kumbe pepa zote alidesa
Au unataka 2010 mapinduzi yawe ya Liberia
Eti utajiri ni mbuga, milima na ziwa Vicktoria
Piga vita ujinga, umasikini na H.I.V carriers
Askofu kutawala nchi hatutaki hizo elimu dunia
Migomo ya chuo kikuu naitupia jicho la 3
Sitetei mpaka Rutashoborwa akiwa wakili kisutu
Kul - nafs - dhal - kal - maut inasema torati
Rest in peace shusha bendera ipepee nusu mlingoti
Bungeni hawaijadili bajeti ya mlala hoi
Mtu hataishi kwa mkate bali neno siyo divai
Tazama timu yako iliyoko madarakani
Na mchunguze kwa makini anayelia sana msibani.

CHORUS

Walimu si mlituahidi mtatupa hela zetu vipiii…?Badooo
Mitihani si mliahidi haitavuja tena….woooooh
Nachingwea na Mbeya vipiii…?Badooo
Tabora…?Badooo
Mtwara…?Badooo
Maisha bora kwa watanzania nyie wenyewe mlituambia
Wamachinga…?Badoooo
Wakulima…?Badooo
Ajira kwa vijana na maendeleo kwa kina mama
Wazee…?Badooo
Vyuo vikuu…?Badooo

VERSE….3

Huu sio wakati wa kuwaua maalbino
Angalau mapinduzi kama Macio Maximo
Usihangaike kumtafuta Roma…mi!! Hakimu wa getho
Mwenye sauti ya mamlaka!!! iliyomfikisha Mrombo Keko
Baada ya kukemea ufisadi na sera za Karamagi
Na waliokula jasho letu kwenye migodi ya Buzwagi
Utazuia vipi ongezeko la wimbi la ukeketaji…
Wakati Ngariba ndo’ diwani wa kata kwenye kijiji!!
Neither do I…!! hongera ulipima ukimwi
Watanzania nasi tuamke tusimpige kibao tu Mwinyi
Hapa nagundua aya-tul - munafik - thalatha
Inawezekana aliishia alifu wakati anasoma madrasa
Huu sio muda wa kujadili kesi za Manji na Mengi
Hayo ya Mungu we Kaisari jadili mambo ya msingi
Teacher alipojiita mtabiri Tanganyika wote vipofu
Padre wa kwanza pentekoste ubatizo wa maji marefu
Machozi yalinitoka Segera watoto hawapati haki
Wengi wamekimbia shule basi lije wauze visheti
Wanaosomeshwa kwa mtaji wa chapati na uvuvi wa samaki
Wabunge wao wamekaa na wanajiita wanaharakati!!
Rudi kwenu kahamasishe nduguzo hawana taaluma
Wazaramo wamegoma soma still mwali wanamcheza ngoma
Wanalia Kilwa Kivinje huku wanaocheka ni wabunge
Walionunua kura ya bibi kwa kumuhonga doti ya kitenge
Hata wamasai walikuchagua kwa kura nyingi za upendo
Wakiamini mtetezi yuaja wa jimbo la Oldoyo Sambo
Waambie what is going on ndani ya himaya ya bwawa la Mtera
Waonyeshe na mikataba ya utawala wa mgodi wa Kiwira
Jeshi lote kwenda Tarime hawakuwa na njia mbadala
Na walioteketea Mbagala!!
Mr.pres …. Haya masikharaaaa!!!
Sina maana utoke wewe hicho kiti umuachie professor
Nisamehe kama nakosea maana mimi sio mwanasiasa
Claps claps claps

OUTRO
By…Mwl...Julius Kambarage Nyerere
Kwa hiyo kitu kimoja tunataka kuelewa…
ni hali ya matatizo ya nchi yetu yalivyo sasa hivi....Eee!!
Kwasababu...sera ya...ay..…awamu ya kwanza…. awamu yangu mimi…
imefanya mema…. imefanya ya kijinga….
ya kijinga yanaachwa…!! lazima yaachwe….
Ubaya wenu ni kwamba…. mnaacha mema...mnachukua ya kijinga.

1 comment:

  1. Oyaa . aliyeiandaa hii lyric shukrani sana kwake kaniiingizia siku tarai. kazi ya masaa matano na zaidi imeenda kwa dak mbili. big up

    ReplyDelete