BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, May 3, 2010

MLELA AJITOA SEREBUKA!!!!!

Star kunako industry ya Bongo Movies,Yusuf Mlela ‘Angelo’, amejitoa kwenye Kinyang’anyiro cha kipindi cha 'Serebuka' ambacho huwa kinachukua nafasi every Tuesday pale Club ya kimataifa ya Billicanas, jijini Dar na kurushwa hewani na Kituo cha Televisheni cha TBC1 kila Jumapili.

Akielezea sababu ya kujitoa kwake, Mlela ana-reveal kwamba sababu kubwa ya kuchukua uamuzi huo inatokana na kuhisi kuwa ndani ya mpambano huo kuna mizengwe na kwamba kuna uwezekano mshindi amekwishaandaliwa.



“Truly nahisi kama kuna mizengwe inaendelea na si ajabu mshindi amepangwa. Kwa mfano wiki iliyopita kabla sijajitoa majaji walinilazimisha nicheze wimbo ambao sijaufanyia mazoezi kwa madai kwamba ule niliokuwa nimeufanyia mazoezi umeshachezwa na mshiriki mwingine, hiyo ni sababu nyingine ambayo ilinifanya nihisi nachezewa rafu.” –alisema Mlela.

No comments:

Post a Comment