BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, January 15, 2010

"HAKUNA KUOGOPA POLISI" NGOMA MPYA YA MADEE

Msanii wa kundi la Tip Top Connection Madee ambaye ni rais wa Manzee jina la paspot, Ahmad Ally amesema kuwa yupo tayari kuachia ngoma yake mpya aliyoupa jina la ‘Hakuna kuogopa polisi’.

Madee alisema kibao hicho kinachozungumzia masuala mbalimbali ya kiusalama amekirekodi katika studio za Dhahabu zinazomilikiwa na msanii Dully Sykes.

Alisema kibao hicho ambacho kinapatikana kwenye albamu yake aliyoitoa mwishoni mwa mwaka jana ‘Pesa’ atakisambaza rasmi kwenye vituo mbalimbali vya redio wiki ijayo.

“Ni kibao kizuri na chenye ujumbe kwa jamii, kama kawaida Madee huwa sibahatishi kazi zangu...mashabiki wangu wasubiri kupata uhondo ndani ya kibao hicho,” alisema.

No comments:

Post a Comment