BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, January 18, 2010

"TUNAJITANUA ZAIDI"- P FUNK

Studio kubwa ya kurekodi muziki nchini Bongo Record iliyopo chini ya Producer maarufu nchini P Funk a.k.a Majani hatimaye imeamua kufanya kitu tofauti kabisa na ndio itakuwa ya kwanza kabisa nchini kuanza kurekodi miziki kwa ajili ya kutengenezea Filamu.

Majani amesema kuwa wameamua kwenda mbele zaidi sio tu kwa kutaka hela anataka awaonyeshe watanzania ni jinsi gani wao kama Bongo Record wanaweza kufanya kitu kingine zaidi ya kurekodi tu.


“Hii ni kitu mpya kabisa nadhani Bongo Record ndio tutakuwa wa kwanza kuanzisha kitu kama hiki, tutakuwa tunafanya kwa Filamu pia na Documentary” alisema P Funk ambaye kwasasa yuko kwenye mojawapo ya kazi hiyo.

Zaidi ya hayo P Funk alisema muziki wa kibongo pia umeingiliwa na umevamiwa na ma producer wengi ni uchwara na ni mojawapo ya sababu ya yeye kufanya kitu tofauti kidogo.


No comments:

Post a Comment