BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, January 28, 2010

'ZINDUKA' WIMBO MPYA WA KAMPENI DHIDI YA MALARIA

Kwa mara ya kwanza wasanii wa Bongo Fleva wamejumuika pamoja na kutunga wimbo kuhamasisha juu ya kujikinga na gonjwa sugu la Malaria.

Ni mkusanyiko wa kwanza ambao haujawahi kutokea katika historia ya muziki wa kizazi kipya kuweza kuwakutanisha wanamuziki kumi tano (15) wa muziki huo wa Bongo Fleva wakiwa wamechanganyikana na wakongwe wengine kwenye muziki huo kama vile Bi Kidude.

“Jina la wimbo unaitwa Zinduka na ni maalumu kwa ajili ya Kampeni za Malaria ambazo zinatarajiwa kufunguliwa na Mheshimiwa Rais mwezi ujao, wimbo wenyewe unawapa tahadhari wananchi kustuka na kuchukuwa kinga zaidi ya gonjwa hilo baya ambalo linaongoza kwa kuua Afrika” alisema mmoja wa wanamuziki aliyeshirikishwa kwenye wimbo huo.

Baadhi ya wasanii waliosimama kwenye songi hilo ni Marlaw, Mwasity, Bi Kidude, Madee, Grace Matata, Ditto, Prof Jay na wengine wengi.




No comments:

Post a Comment