BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, January 14, 2010

WOTE FEKI, MIMI NDIO ZAIDI YAO- RAY C

Mwanadada wa siku nyingi kwenye game la muziki wa kibongo Rehema Chalamalia a.k.a Ray C ameibuka na kusema hata waje wasanii wangapi wa kike lakini anaamini hakuna kama yeye kamwe na hakuna atakayekuja kuyafikia mafanikio yake.
Ray C au kama anavyojulikana kwa jina lingine kiuno bila mfupa aliyasema hayo baada ya siku za karibuni kuibuka wasanii wengi wa kike na kila mmoja kujitamba kwamba yeye ni zaidi ya wengine wote.
“Unajuwa watu wakikuona umekaa kimya wanadhani labda unawaogopa au vipi?, hawajui hata mtu kuwa unafanya nini, ni kweli kwa kipindi kirefu nilikuwa kimya lakini nilikuwa nafanya mambo yangu mengine nje ya nchi ambayo hayahusiani na muziki kabisa, basi wameibuka wengi na kashfa kibao, sasa nataka kuwaambia ya kuwa inatosha, na rasmi wajuwe kuwa mwaka 2010 nitakuwa kimuziki zaidi” alisema Ray C.

Ray C akiongea kwa hasira alizidi kusema “Lakini mimi hakuna demu wa kunitisha hapa Bongo si kwenye muziki sehemu yoyote ile, mi muziki nimefanya kipindi kirefu sana na mpaka sasa hakuna anayeweza kujifananisha na mimi, hakuna ambaye ameweza kufikia kiwango changu bado nipo mbali sana ndio maana napata shoo nyingi hata nisipotoa kazi mpya, nyimbo zangu hazichuji ukisikiliza ‘Na Wewe Milele’ sasa hivi hapo ulipo lazima usisimke lakini ni ya miaka mingi.” alimaliza Ray C


No comments:

Post a Comment