BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, January 11, 2010

MAPINDUZI ZAIDI YA FILAMU 2010- ASEMA ADILI

Mmoja wa wanamuziki waanzilishi wa Bongo Fleva miaka ya nyuma Adili Mkwela ambaye aliachana na kuimba na kuamua kujikita zaidi kwenye mambo ya Production ameibuka na kusema mwaka huu analeta mapinduzi katika Filamu za kibongo.

Adili aliyasema hayo wakati wa utambulisho wa Filamu yake Mpya inayokwenda kwa jina la Loleza ambayo kwa kupitia kampuni yake mwenyewe ndio wamefanya kazi nzima. “Ni filamu mpya iliyochezwa na wasanii maarufu kama vile Mansu-Li, Buff G, na wengine kibao, kupitia kampuni yake ya Chapakazi Filmz,” alisema Adili
Nyota huyo wa rap amesema filamu hiyo inakuja kuonyesha upande wake wa pili wa kipaji na anasema “Loleza ni filamu unayopaswa kuitazama”.

“Angalia kuanzia kasha lake hadi upigaji picha kusema kweli ina ubora wa hali ya juu sana, tuna uhaba wa maeneo ya kupigia picha lakini tuliliangalia hilo na tumejitahidi kwa kiasi kikubwa kupata maeneo mazuri kwa kazi hiyo” alisema.

“Nimetumia miaka mitatu ku-plan mambo haya, ndio maana watu wakaona kama niko kimya, lakini nipo miaka yote nikipanga mageuzi katika filamu na majibu ni haya.” alimaliza kusema


No comments:

Post a Comment