
Meneja wa uhusiano wa Multichoice Furaha Samalu alisema kwamba Lilian amefanikiwa kupita hatua ya kumi (10) bora baada ya kupita mchujo wa washiriki wengine 24 kutoka nchi mbali mbali.

Lilian anatarajiwa kuondoka tarehe 26 kuelekea Afrika Kusini tayari kwa fainali hizo ambazo zinatarajiwa kufanyika nchini Nigeria katika mji wa Lagos.

Lilian ni mwanafunzi katika chuo kikuu cha Dar es salaam amewaahidi watanzania kufanya makubwa na kufwata nyao za dada yake Miriam Odemba kama ilivyokuwa mwaka 1999.
No comments:
Post a Comment