BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, June 14, 2010

D KNOB AKANA MATUSI!

Inocent Sahani a.k.a D Knob ameibuka na kukanusha habari zilizoandikwa na gazeti moja litokalo kila wiki mara mbili kuhusu shutuma za kuwa wabongo wamem-diss.

Kwa njia ya ujumbe mfupi wa maandishi wa simu D Knob alisema hata siku moja hawezi kuwa - diss wabongo kwani bila wao yeye asingekuwepo alipo leo hii na kwa mantiki hiyo hizo habari hazina ukweli wowote nakanusha kabisa.

Ujumbe wenyewe unasomeka kama ifuatavyo “Napenda kutangaza kuwa sijafanya interview na mwandishi wa habari yeyote hivi karibuni kwa hiyo nakanusha habari iliyoandikwa na gazeti la ijumaa la wiki mbili zilizopita kuwa wabongo wananidisi. Bila wabongo nisingekua hapa nilipo na wananisapoti na ndio maana Napata moyo wa kufanya vizuri” alisema D Knob

No comments:

Post a Comment