BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, June 14, 2010

'MBWELA'- CHIFU WA KWANZA WA WAZIGUA KUTIA SAINI MKATABA NA DK. KARL PETERS!

Dk. Karl Peters (kati) akiwa na wenzake Dk. Karl Juhlke na Joachim Graf. Huyu Dk. Karl Peters ndiye aliyewaingiza mkenge babu zetu wakati wa kuingia ukoloni wa Ujerumani nchini kwa kuingia katika mikataba ya kilaghai na watawala wetu wa jadi.

(Mbwela, Chifu wa Wazigua mkoani Tanga, ndiye aliyekuwa mtawala wa jadi wa kwanza kutia saini mkataba na Dk. Karl Peters mwaka 1884.)

Haya na mengi mengineyo yanayohusu historia ya nchi hii yanapatikana katika Makumbusho ya Taifa jijini Dar ambako kwa sasa ukarabati wake unakaribia tamati ili kuifanya sehemu hiyo isiwe tu ya makumbusho bali sehemu ya kukutania wadau wakubwa kwa watoto, wake kwa waume kwa shughuli mbalimbali ikiwemo utamaduni, sanaa na mengineyo.

Makumbusho hiyo ya Dar (katikati ya jiji karibu na IFM na sio Kijiji cha Makumbusho Kijitonyama kama ambavyo wengi wamezoea kuchanganya) hivi sasa inajulikana kama Makumbusho na Jumba la Utamaduni - Museum and House of Culture.

Asante MICHUZI

No comments:

Post a Comment