BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, June 21, 2010

'MECHI ZA UGENINI' NGOMA MPYA YA ROMA FT JOSE MTAMBO!!

Mkali wa Hip Hop kutokea Tanga Town, Rymes Of Magic Attraction a.k.a ROMA, ameachia ngoma nyengine mpya inayokwenda kwa jina la 'Mechi Za Ugenini' aliyomshirikisha Jose Mtambo, ikiwa imeitengeneza pale Tongwe Record.

Roma ambaye pia amewahi kutajwa kwenye tuzo za Teen Extra Award za Clouds Fm, mpaka sasa anatamba na ngoma zake nyengine kama na 'Mr President' pamoja na 'Pastor' ambazo hadi sasa bado zinafanya vizuri kunako vituo vya redio.

Isikilize ngoma hiyo mpya ya 'MECHI ZA UGENINI' hapo kulia juu palipoandikwa SIKILIZA TANGA FLAVA HAPA!


No comments:

Post a Comment