BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, April 12, 2010

MISS TANGA 2010 YAZINDULIWA RASMI!

Wakurugenzi wa kampuni ya 5 Brothers Entertainment Asma Makau na Nassoro Makau wakizindua rasmi mashindano ya urembo ya Miss Tanga kwa ngazi ya vitongoji, ambapo kwa safari hii kutakuwa na vitongoji saba tofauti na mwaka jana. Vitongoji hivyo ni Miss Usagara, Miss NGamiani, Miss Chumbageni, Miss College, Miss Tanga City Central, Miss Lushoto na Miss Pangani ambayo inaandaliwa na Anko Mo Blogspot.

Wachangia mada mbali mbali wakati wa uzinduzi wa Miss Tanga. Bra A wa Mwambao Fm na Mimi (Anko Mo) wakati nawakalisha mchango wangu kunako Hoteli ya Kola Prieto iliyopo katikati ya jiji la Tanga.

Warembo wakifuatilia hoja za wajumbe wengine kwa makini zaidi.

Tina wa kwanza, ambaye anandaa Miss Usagara akiwa na Raymond Minja kutokea Mwambao Fm na huyo aliyekunja swala anaitwa Paulina Mgonja.

Wadau wa urembo wakiwa makini katika kusikiliza, mama Sophia Production na wadau wengine.

Mdau mkubwa Miss Tanga ambaye pia ni mwandishi wa gazeti la Mwananchi Burhan Yakub akigawa mikataba kwa waandaji wa Miss Vitongoji.

Muandaaji wa Miss Chumbageni dada Suzy akiwa na mwandishi wa gazeti la Bingwa na mtangazaji wa Mwambao Fm Oscer Assenga, wakati wa uzinguzi wa Miss Tanga.

Warembo wakizungumza kitu punde baada ya uzinduzi huo kumalizika.

Watangazaji wa Breeze Fm Benson na Amir wakiiwakilisha redio yao. Breeze Fm inandaa Miss Ngamiani. Kauli mbiu ya Miss Tanga 2010 ni "Its Wonderful Event"

No comments:

Post a Comment