BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, April 8, 2010

TULIPOTOKA NA TUNAPOKWENDA!

Tulichofanya ni kuongeza "SIFURI MBILI" (00). Kwahiyo miaka ijayo tukiongeza tena mbili basi tutakuwa na karatasi ya milioni moja!!! Na hii itakuja kama hatutajibihidisha kuuza pamba, kahawa, chai n.k. kwa wingi zaidi nje. Sasa hivi hakuna tena uwiano wa kati ya export na import kwa sababu tumeamua iwe hivyo baada ya kuwapuuzia wakulima wetu wa mazao ya biashara na kuviua hata vile viwanda vyetu, kama vile vya nguo.

Badala yake sasa tuna wajasilimali wengi wanaokwenda China na kwengineko kutuletea bidhaa ambazo tungeweza kuzitengeneza wenyewe kwa malighafi tuliyonayo. Ni aibu kila ninapoona hata vijiti vya kusafishia meno(toothpicks) tunaagiza nje... Kile kiwanda cha vibiriti cha Kibo vipi?

Ikiwa kama madini yote tumewapa wajanja, sisi tumebaki na nini cha kuweza kutuinua? Au utalii ambao bado kuutangaza ipasavyo?

Uchaguzi unaokuja uwe ni uchaguzi wa kuwauliza wagombea ni nini wataifanyia Tanzania?

Asante Fundi Wa Kombo

No comments:

Post a Comment