BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 7, 2010

PANGANI INAVYOZIDI KUPIGA HATUA KATIKA ELIMU!

Sheikhe mkuu wa Baraza kuu la waislam Tanzania BAKWATA Sheikhe Isa Saabani Bin Simba akiweka jiwe la msingi leo katika ujenzi wa shule ya sekondari inayojengwa na BAKWATA eneo la Mkoma Wilayani Pangani kwa ufadhili wa benki ya dunia ya kiislam.

Sheikhe Isa Saabani Bin Simba akitazama kwa makini kibao kinachoonyesha kuwa ni yeye ndie aliyeweka jiwe hilo la msingi.

Sheikhe Isa Saabani Bin Simba akisindikizwa na baadhi ya viongozi wa BAKWATA mkoani Tanga wakati anakwenda kuweka jiwe la msingi.

Kama unavyoona pichani.

Viongozi wa BAKWATA wakimkaribisha naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi Mh Mwantumu Mahiza wakati wa uwekaji wa jiwe la msingi katika sekondari mpya wilayani Pangani mkoani Tanga.

Mh Mwantumu Mahiza akisema jambo kwa wakazi wa Pangani waliohudhuria hafla hiyo.

Sheikhe Isa Saabani Bin Simba nae akisema jambo.

Waumini wa dini ya kiislamu wakiwa makini wakifuatilia yaliyokuwa yanasemwa na viongozi wao.

Karibu mgeni! Sheikhe Isa Saabani Bin Simba akikaribishwa Pangani.

Sheikhe Juma Luuchu akikaribisha wageni

Picha wa pamoja na baadhi ya viongozi wa BAKWATA!

No comments:

Post a Comment