BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, April 9, 2010

SANAA INAVYOZIDI KUCHUKUA KASI JIJINI TANGA!

Muuzaji wa sanaa mbali mbali za michoro, ushanga, nguo, mabegi, mikanda, picha za ukutani n.k akipanga vitu vyake kabla ya kuanza kazi.

Baadhi ya sanaa zinazopatikana kwenye duka lake. Yupo chini ya jengo la Club La Casa Chica, karibu na ofisi za Zantel.

Vijago kama vinavyoonekana pichani. Inaonyesha ni jinsi gani alivyo mbunifu.

Ushanga na baadhi ya urembo mwenigne wa sanaa vikiwa dukani.

Nilipomuuliza imekuwaje hadi ukaamua kufanya biashara hii ya sanaa- akanambia kuwa Tanga ya leo sio ya kipindi hicho. Mji umekuwa na watu wanafurahia bidhaa zake.

Vyote hivi ni kazi ya mikono yake.

Wageni na wenyeji mnakaribishwa kununua sanaa za Tanga.

Picha safi kwa ofisini na nyumbani pia.

Karibuni Tanga!

No comments:

Post a Comment