BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, April 7, 2010

SERIKALI YARIDHIA ALBAMU YA WAGOSI WA KAYA

Wakali wa maneno ndani ya Sanaa ya Muziki wa Kizazi Kipya, Fred Malick ‘Mkoloni’ na Dk. John wanaounda Crew ya ‘Wagosi wa Kaya’ wameibuka na kuipigia makofi hatua ya serikali kuruhusu kwenda kitaani kwa albamu yao mpya ya inayokwenda kwa jina la ‘Miaka Kumi ya Maumivu’ iliyokuwa imepigwa stop awali.

Akiongea hivi karibuni, katikati ya wiki iliyopita, Mkoloni ambaye ni mmoja wa wasanii wa kundi hilo, alisema sababu ya kufungiwa mwanzoni ilikuwa ni kuwepo kwa baadhi ya nyimbo ndani ya albamu hiyo, zenye mashairi yanayohofiwa kuchochea vurugu wakati wa Uchaguzi Mkuu, baadaye Oktoba mwaka huu.

“Tulilazimika kukubaliana na agizo la serikali na kubadili aina ya maneno tuliyokuwa tumeyatumia ili kupata baraka za kupeleka mzigo sokoni na hatimaye tumefanikiwa,” alisema Mkoloni.

Akaongeza: “Naamini hadi serikali imekuwa makini kuangalia albamu nzima, basi wanafahamu moto wetu.”

No comments:

Post a Comment