BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, June 21, 2010

ANNA KIWAMBO NDIO MISS TANGA 2010!!!!

Mnyange wa Miss Tanga 2010 Anna Kiwambo akiwa katika uso wa furaha punde tu baada ya kutangazwa kuwa mshindi katika mchakato huo uliofanyika katika hoteli ya Tanga Beach Resort iliyopo Sahare, Miss Tanga 2010 imeandaliwa na 5 Brothers Entertainment.

Anna Kiwambo akiwa na washindi wengine, mshindi wa pili alikuwa ni Jari Mure, wa tatu ni Zuleha Mrisho. Nafasi ya nne alichukua Asia Gumbo na nafasi ya tano alinyakua Grace Joseph.

Matonya aki'show love kwa Miss Tanga 2010.

Hii ndio Tano Bora ya Miss Tanga 2010. Majaji walifanya kazi nzito hadi kufikia hapa.

Hii ilikuwa kumi bora.

Warembo wa Miss Tanga wakiwa wamejipanga na vazi la jioni.

Walimbwende katika show.

Miss Tanga 2010- its a wonderful event!!

Katika hali iliyofanya mashabiki wengi wainuke kwenye viti vyao na kushangilia, ni pale Aziza Khalifa ambaye pia ni Miss Pangani 2010 alipotangazwa kuwa mnyange wa Miss Talent Tanga 2010. Miss Pangani 2010 iliandaliwa na blog hii.

Aziza akiwa kwenye uso wa furaha baada ya kuvishwa taji la Miss Talent.

Matonya alikuwepo, japokuwa alipiga show dakika za mwisho.

Ney wa mitego karibu tena Tanga. Ulifanya kazi nzuri kaka.

Mrembo aliyekuwa anamaliza muda wake Glory Chuwa ambaye ni Miss Tanga 2009 akiwa katika tabasamu nono.

Glory akitoa neno la mwisho kwa watu wliohudhuria Miss Tanga 2010.

Kulikuwa na burudani nyingi....huyu jamaa anafanya yoga hapa! Alishangaza watu kwa staili zake za kujikunja.

Hapa sikujua alikaaje jamani..alikuwa anatembea kama yule mdudu tandu!!

Tanga Beach Resort ipo full..maswala ya misosi kwa waliokaa VIP ilikuwa safii!

Majaji wakiwa makini na kazi yao.

Lilian Mdachi akiwa amemkumbatia mshiriki wa Miss Tanga 2010, pamoja na mkali wa kiduku- akida a.k.a kijogoo.

Nilipenda washereheshaji walivyovaa, ulikuwa ubunifu wa hali ya juu. Walivaa kipwani hasa.

Watu wakipata burudani.

Huku ni karibu na back stage...tulikuwa wengi eneo hili.

Wadau wa mashindano ya urembo jijini Tanga, Benedict Kaguo ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la majira, na pia mtangazaji wa redio Mwambao Fm ya jijini Tanga. Halikadhalika Oscar Assenga, mtangazaji wa Mwambao Fm na pia ni mwandishi wa gazeti la Bingwa.

Nyuma ya stage...Amina aliyenyoosha mkono. Ndie alikuwa ni mwalimu wa Miss Tanga. Walimu wengine ni Mariam Bandawe na Oliver, hawapo pichani.

Swahiba wangu wa ukweli..Dj Bob Nass wa Breeze Fm Radio ya jijini Tanga akiwa na mshkaji wake.

Daaah! Huyu jamaa anaonekana ni mnoko ile mbayaa- tazama alivyoishika hiyo Camera..! Ila kazi nzuri, anatokea Sofia Production.

4 comments:

  1. Haa! Jamani..... Mbona miss Tanga ana kitambi?

    ReplyDelete
  2. labda majaji wamepewa rushwa

    ReplyDelete
  3. Nadhani miss Tanga amepewa tu ili kuhitimisha.Ni kweli ana kitambi na sijui kama atafika mbali.

    ReplyDelete
  4. HUYO MISS NI KIMEO SI KITAMBI TU, HIYO PUA JE? HAMUONI KAMA NI KUBWA, HATA MIMI NINA WASIWASI

    ReplyDelete