BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, July 19, 2011

KIJANA AANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU AKIJARIBU KUKWEPA NYAYA ZA UMEME

Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, alianguka na kupoteza fahamu katika eneo la Gofu hapa jijini Tanga karibu kabisa na ofisi za mkuu wa mkoa. Kwa mujibu wa wapita njia wengine waliomuona wakati anaanguka, walidai kuwa kijana huyo alikuwa akijaribu kukwepa nyaya za umeme zilizokuwa zimeanguka barabarani. Tukio hilo lilitokea siku ya jana majira ya saa mbili asubuhi.

Wasamaria wema wakimtazama kijana aliyeanguka huku wakijadili namna ya kumsaidia.

Mzee huyu alijitoa mhanga kwa kuzitoa nyaya za umeme zilizoanguka barabarani na kufanya kijana huyo kuanguka na kupoteza fahamu. Mpaka naondoka eneo la tukio, kijana huyo aliweza kupata msaada na kupelekwa hospitali ya Bombo.

No comments:

Post a Comment