BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, July 21, 2011

HATIMAE JAIRO KIBARUA KIMEOTA NYASI!

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, amesimamishwa kazi rasmi kufuatia kutangazwa rasmi habari hizo na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemo Luhanjo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma.

Kutimuliwa kazi kwa Jairo kumekuja baada ya Beatrice Shelukindo mbunge wa Kilindi Mkoani Tanga kulipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini juu ya kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.

No comments:

Post a Comment