
Thursday, July 28, 2011
VIJANA WA TANGA TOWN!

Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Wednesday, July 27, 2011
ALBINO KUPANDA MLIMA KILIMANJARO

Anatarajia kuanza safari yake hiyo itakayomchukua siku nane, Jumamosi wiki hii kuelekea kileleni kwa lengo la kuithibitishia jamii ambayo bado inaendeleza vitendo vya ukatili na unyanyapaa dhidi ya albino kwamba wao wanaweza kufanya kila kitu.
Torner ametoa kauli hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari na kusema lengo pamoja na kufikisha ujumbe huo muhimu ni kuwa albino wa kwanza Tanzania kufanya kitendo hicho cha kishujaa cha kufika kwenye kilele cha Kilimanjaro, mlima mrefu barani Afrika.
“Nipo mbele yenu hapa leo kuweka msimamo dhidi ya mawazo potofu yaliyopo katika fikra za baadhi ya Watanzania na Waafrika wengi ambao wanaamini kwamba albino hana uwezo sawa na watu wengine, fikra hizi ni hatari zimeendelea kusababisha ubaguzi, kutengwa, ukatili na mauaji dhidi yetu kwa muda sasa,” amesema.
“Jumamosi ya Julai 30, mwaka huu, nitaanza safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro lengo kuu ni kufikisha haki za albino kileleni mwa Afrika na kutangaza kwa sauti kubwa niwezavyo kwamba albino sio mtu wa kuogopwa, kubaguliwa, anayestahili kuwindwa kama mnyama wa porini akikatwa vipande kwa ajili ya biashara, bali ni binadamu kama wengine.”
Torner amebainisha kuwa, uamuzi wake huo umetokana na kasi ya vitendo vya ukatili na mashambulizi yanayoendelezwa na baadhi ya Waafrika kutokana na imani za kishirikina zilizochochea biashara ya viungo vya albino na kusababisha madhara mengi kwao hasa kulazimishwa kuishi kwa wasiwasi.
“Nitakapopanda mlima nitapanda kwa ajili ya albino wote waliolazimishwa kuondoka nyumbani kwao kwenda kuishi kwenye kambi maalumu zinazowatenga na familia zao na kuwapa upweke na kuwaambia iwe mwisho wa kujificha kwenye kivuli cha jua tena, ndoto yangu ni kuunganisha albino wote ili tuuthibitishie ulimwengu tuna uwezo sawa na binadamu wengine ila tunatofautishwa na mahitaji,” amesema.
Takriban miaka mitano sasa, hali ya albino nchini imekuwa si shwari kutokana na kasi ya ushambuliaji, uwindaji na mauaji ya kikatili yaliyosababisha vifo zaidi ya 60, huku Serikali ikilazimika kuhamisha wanawake na watoto 118 katika shule maalumu ili kuimarisha ulinzi na usalama wa maisha yao dhidi ya wawindaji.
Na Anna Makange, Tanga.
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Monday, July 25, 2011
PROFESSOR JAY AND DITTO MEET WITH STUDNETS IN TANGA USING PERFORMANCE TO FIGHT MALARIA
The judges were treated to a spectacle of talent as they witnessed an array of performances including poetry readings, songs and even theatrical performances
On reaching the final round, Tanzanian artist, Ditto, took to the stage to talk to the students about how important it is to protect themselves from malaria to ensure they secure their future, before the artist sang the malaria he had written for the Zinduka! campaign which has now become an anthem for a generation fighting against malaria.
The students were then surprised when another guest Bongo fleva rapper and Zinduka! goodwill ambassador Professor Jay joined Ditto on stage to sing the anthem.
The artist has been a prominent figure in the fight against malaria, featuring in the launch of the Zinduka! campaign in 2010 and making regular appearances for the campaign in the field and on TV.Professor Jay then took time to hand out awards to the lucky competition winners.
The artist has been a prominent figure in the fight against malaria, featuring in the launch of the Zinduka! campaign in 2010 and making regular appearances for the campaign in the field and on TV.Professor Jay then took time to hand out awards to the lucky competition winners.
Professor J had this to say, “I joined the Zinduka! campaign with the hope that through my music I could help to fight malaria in Tanzania. But to see kids wanting to get involved and using music as the platform to fight malaria in their communities, that’s what makes me most proud of the work we have done.
Professor Jay and Ditto then invited youth to join him as he visited a number of houses near Tanga town, where the youth spoke to households about what measures they use to protect themselves from malaria and what they think needs to be done to eradicate malaria in Tanzania.
The Malaria Haikubaliki Campaign is led by the Tanzanian Government behind the leadership of President JakayaKikwete. It is supported by partners including Malaria No More, Tanzania House of Talent (THT), Johns Hopkins University, Population Services International and United Against Malaria. The goal of the program is to achieve universal bed net coverage and eliminate malaria deaths by urging all Tanzanians to Zinduka! (“Wake up!”) to the threat of malaria and protect themselves against the disease
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
SERENGETI FIESTA 2011 NI FULL MAJOTROOOOO
Wananchi wa Tanga wakifurahia Serengeti Fiesta 2011 iliyofanyika jijini Tanga siku ya jana Jumapili ya tarehe 24/07/2011 kwenye uwanja wa Mkwakwani......hakika ilikuwa bonge moja la show! wakazi wa Tanga walijitokeza wka wingi na majatrooo yaliwabamba vilivyo.
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Thursday, July 21, 2011
HATIMAE JAIRO KIBARUA KIMEOTA NYASI!

Kutimuliwa kazi kwa Jairo kumekuja baada ya Beatrice Shelukindo mbunge wa Kilindi Mkoani Tanga kulipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu huyo wa zamani wa Wizara ya Nishati na Madini juu ya kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Wednesday, July 20, 2011
HAWA NAO WATAKUWEPO KWENYE SERENGETI FIESTA 2011 PALE MKWAKWANI SIKU YA JUMAPILI









Labels:
Mwandishi: ANKO MO
SHELUKINDO ALIVYOFUNGUKA BUNGENI!

Beatrice Shellukindo amelipua bomu Bungeni akimtuhumu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, kwa kutumia zaidi ya Sh 1 bilioni kwa ajili ya kutoa rushwa kwa watu mbalimbali ili bajeti ya wizara hiyo iweze kupitishwa na Bunge.
Tuhuma hizo nzito zinakuja kipindi ambacho tayari Wabunge wa Kamati ya Nishati na Madini wakiwa wameibua tuhuma kama hizo za baadhi ya wajumbe kutaka kuhongwa na maofisa wa wizara hiyo, ili kurahisisha upitishaji wa bajeti ndani ya kamati.

Takriban wiki tatu tangu wabunge wa kamati hiyo kuibua tuhuma hizo ambazo zilifika hadi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, hivi juzi tena Shellukindo alikoleza moto huo wakati akichangia bajeti ya wizara.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda alikubaliana na tuhuma hizo. Akitoa hoja ya kuondoa bungeni hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini, Pinda alisema alikuwa akisubiri Rais Jakaya Kikwete afike Afrika ya Kusini alikokwenda katika ziara ya kiserikali ili aweze "kumshtaki" Katibu Mkuu huyo kutokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yake. Pinda alisema hawezi kuchukua hatua dhidi ya Jairo kwani kwa mujibu wa sheria, mamlaka ya uteuzi ndiyo inayoweza kuchukulia hatua dhidi yake.
Beatrice Shelukindo ni mbunge wa jimbo la Kilindi mkoani Tanga kupitia chama cha mapinduzi.
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Tuesday, July 19, 2011
SERENGETI FIESTA 2011 INAKUJA TANGA JUMAPILI YA TAREHE 24/07/2011


Labels:
Mwandishi: ANKO MO
KIJANA AANGUKA NA KUPOTEZA FAHAMU AKIJARIBU KUKWEPA NYAYA ZA UMEME



Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Monday, July 18, 2011
TIMU YA DALADALA ILIVYOFANYA KAZI YA KUREKODI VIPINDI MKOANI TANGA


(Pichani mimi na Daniel Kijo, mtangazaji wa kipindi cha daladala)

(Pichani Daniel akiwa na mdau wa kipindi cha daladala, barabara ya nane)

(Timu ya kipindi cha daladala wakiwa na afisa elimu Kombo wakati wa kuelekea kurekodi)

(Daniel kwenye bustani za Tanga)














(Timu nzima ya Daladala iliyokuwepo jijini Tanga ni pamoja na Dani Kijo na Bi Kiroboto ambao ni watangazaji. Wengine ni Eldad Mark Film Director, Emanuel Zing Driver, Deogratius Sizya Camera man, Tanya creative producer, Anton second driver na Steve Martin researcher.)
Labels:
Mwandishi: ANKO MO
Subscribe to:
Posts (Atom)