BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, February 19, 2010

ROGGER ARUDI NA TASWIRA MPYA YA MUZIKI!

Mwanamuziki wa Bongo fleva aliyekuwa miongoni mwa waliofanya vizuri shindano la Bongo Star Search (BSS) ya 2008, Rogger Lucas, ambaye alikuwa kimya kwa muda mrefu ,amerudi na kitu kipya chenye sura tofauti na tuliyoizoea.

Tulizoea kumuona akiimba peke yake au akishirikiana na msanii mwingine (featuring) ila kwa sasa ameibuka na kikundi chake kipya kiitwacho MOTHERLAND. Bendi hii imesukwa nchini uholanzi chini ya udhamini wa bendi iitwayo ROOTS RIDERS yenye maskani yake huko huko Uholanzi lengo likiwa kuwasaidia wasanii kutoka Afrika katika fani ya Muziki.

Rogger amewataka mashabiki wake kuwa wavumilivu kwani hivi karibuni anatarajia kuingia sokoni rasmi akiwa na bendi yake hiyo katika kumbi mbalimbali za starehe kama ambavyo bendi nyengine za Tanzania zimekuwa zikifanya.

Ameweka bayana kuwa bendi yake inaundwa na wasanii kibao wakiwemo wakongwe na chipkizi kama; Ozeey, Grace Matata, Njuu a.k.a Crista Bella. Kala Jeremiah, na wengine wengi. Kwa sasa msanii huyo anatarajia kutoa video ya wimbo uitwao JASHO LA UPENDO kabla ya kuanza kazi rasmi na bendi yake hiyo.

Kwa habari zaidi bofya hapa



No comments:

Post a Comment