
Katika nyimbo hizo.Bwagamoyo inataraji kurekodi pia wimbo unaotazamiwa kuwatoa machozi wasikilizaji na watazamaji wa televisheni, ujulikanao kwa jina la Nafsi haina urithi ambao unawataja watu mbalimbali waliokwishaaga dunia akiwamo Rashid Kawawa .

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika kambi ya Jijini Tanga, Mkurugenzi wa Bwagamoyo,Muumini, alisema bendi hiyo imeasukwa upya kwa lengo la kuleta ushindani katika soko la muziki huo nchini na nje ya nchi .
Alizitaja nyimbo zitakazorekodiwa kuwa ni Mwanamtili Malunde na Nafsi haina urithi zilizotungwa nay eye Muunimi akishirikiana na Dr Rama,pamoja na Undugu wa mashaka ukiwa ni utunzi wa Venance Joseph ambaye pia ni Rais wa bendi hiyo inayotumia mtindo wa gusa unase.

“Bwagamoyo International imesukwa upya inao wanamuziki mahiri waliojiunga kutoka bendi nyingine na pia imepata wanenguaji tishio”alisema Muumini na kusita kuwataja kwa maelezo kuwa baadhi yao hawajakamilisha mipango ya kutoka kwenye bendi zao za awali.

Gitaa la solo linakung’utwa na Hemed Yassin,Yahaya Makango (Rhyizi)m,na George Gama (Bass) na Keybody Kally huku Drums na tumba zikipigwa na Patrick Clayery na Hamza Salehe. .

Bendi hiyo imejizolea mashabiki baada ya kufanya ziara katika mikoa ya Kanda ya ziwa ambako ambako miongoni mwa nyimbo zilizopigwa ni Tunakukumbuka mama,Manyanyaso yatima,undugu wa mashaka,Nani kama mama,Natafuta mume na Quity baby.

HABARI NA OSCAR ASSENGA
No comments:
Post a Comment