BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, March 30, 2010

TATIZO HAWAJUI KUANDIKA- MASTER J

nini haswa kinachowafanya wale nyota wa taji kubwa la Bongo Star Search BSS kila mwaka...kushindwa kuwika kwenye soko la muziki kama ambavyo wengi wetu tunategema,mmoja wa majaji wa tuzo hizo na akiwa mmoja wa Maprodyuza walioishep Bongo Fleva wakati inasimama na kukubalika pamoja na aina nyingine ya muziki anasema sababu kubwa la nyota hao kutoonyesha cheche sokoni ni kwasababu hawawezi kuandika.

“Tatizo si BSS, Benchmark, Madam Rita wala majaji, tatizo ni wasanii wenyewe kwa sababu hawana uwezo wa kuandika na kuandaa nyimbo zao ili zikubalike. “Wasanii wanaposhiriki BSS, wanaimba nyimbo za watu, kwahiyo wanaonesha uwezo wao kwa kuimba tu, hivyo wanakubalika na wanapigiwa kura lakini kwenye kutunga hakuna.

“Hii ndiyo sababu Jumanne Idd (mshindi mwaka 2007), Misoji Nkwabi (2008) wameishia njiani, unaona hata Pascal Cassian (2009) bado hajasimama, angalau Peter Msechu (1st runner up 2009) anaokoa jahazi.

“Nilitoa ofa ya wasanii wote walioingia Top 5 kurekodi nyimbo kwenye studio yangu (MJ Production) ili kuonesha mwanga ili Watanzania waone kwamba kumbe inawezekana Staa wa BSS akawa mfanyabiashara mzuri wa muziki nchini.

“Hilo tumeliangalia kwa mapana na mikakati ya BSS mwaka huu ni pamoja na kutafuta watu watakaowaandikia nyimbo washindi na kuwachagulia ala, kwahiyo baada ya shindano wataingia studio na kufyatua mawe yenye akili.”

No comments:

Post a Comment