BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, November 8, 2010

ANKO MO BLOGSPOT YAJA NA POLL NYENGINE!! "JE TANGA NI JIJI..??!"

Napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wale wote walioshiriki kupiga kura kupitia Poll ya Blog ya Vijimambo Vya Tanga. Poll iliyokuwa inahusiana na maswala ya uchaguzi mkuu 2010, kuwa chama gani kingeweza kushinda.

Mpaka mwisho matokeo yalionyesha kama ifuatavyo, CCM 25.38% (33 votes), CHADEMA 61.54% (80 votes), CUF 10% (13 votes), NCCR 3.08% (4 votes) na jumla ya kura zote zilikiuwa 130. Matokeo haya ni kwa mujibu wa kura uliyokuwa unapiga kila siku.

Ilikuwa ni changamoto tu, ili kuweza kupata mawazo tofauti ya watanzania katika swala zima la siasa. Nawashukuru tena na tena kwa kuchukua muda wenu na kushiriki. Ila uchaguzi umekwisha na Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ndio ameibuka (Rais) kidedea kwa mara ya pili tena.

Kama kawaida Blog yako ya VIJIMAMBO VYA TANGA haichoki kuchemsha bongo yako. Safari hii inataka kujua, JE TANGA NI JIJI..?? piga kura kwenye NDIO, HAPANA au SIJUI! Natumai nyote mmekuwa mkiona picha za Tanga. Hebu toa mawazo yako kwa kupiga kura hapo pembeni kulia palipoandikwa KURA YAKO HAPA!!. Asanteni sana.


No comments:

Post a Comment