BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, November 2, 2010

MCHEZO UMEKWISHA!!!! NUNDU AICHUKUA TANGA MJIN!!

MSIMAMIZI wa uchaguzi wa jimbo la Tanga, John Gikene amemtangaza rasmi Omari Nundu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mbunge wa Jimbo la Tanga baada ya kupata ushindi wa kishndo kwa kuzoa kura 40,225 na hivyo kuwabwaga wagombea wa vyama vya upinzani waliokuwa wakiwania jimbo hilo.

Chama cha Wananchi (CUF) kupitia mgombea wake Musa Mbarouk kimeambulia kura 24,262 na kufuatiwa na Kassim Amar wa (CHADEMA) aliyepigiwa kura 5750, ambapo jimbo hilo la Tanga jumla ya watu 1,79,200 walijiandikisha kupiga kura.

Hata hivyo waliojitokeza kupiga kura katika jimbo hilo ni 72,192 ikiwa ni sawa na asilimia 40 ya waliojiandisha ambapo kura halali zilikuwa 70,666 na zilizoharibika zilikuwa ni kura 1526.


Na Sophia Wakati, Tanga

No comments:

Post a Comment