BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, August 24, 2010

DEEP SEA- SOKO MAARUFU KWA SAMAKI JIJINI TANGA

Hawa ni baadhi ya samaki wazuri wanaopatikana Deep Sea, moja ya soko linalouza samaki kwa bei nafuu kabisa. Wachuuzi wengi wa samaki jijini Tanga huja hapa na kununua kwa jumla na kisha kusambaza majumbani. Ni eneo la baharini, lipo katikati ya Chumbageni na Kisosora

Samaki wakiwa kwenye meza tayari kwa kuuzwa.

Nilinunua hilo fungu la kwanza kwa ajili ya kitoweo wadau....

Wauzaji wa samaki wakiwa makini katika biashara yao.....hapa alikuwa akizungumza na mteja.

Kwa kipindi hiki cha Ramadhani samaki wamekuwa wakiuzika kwa wingi kutokana na kutumika sana kama kitoweo cha Daku pamoja na Muhogo wa Nazi.

Meza nyengine ikiwa na samaki. Hapa kila dakika samaki huletwa, tena wengine wakiwa bado hai.

Wakazi wa Tanga wakiwa katika harakati za kununua samaki eneo la Deep Sea.

Hii njia inaelekea chini sehemu ambayo kuna bahari na vyombo vya uvuvi wa samaki.

Ukiwa Deep Sea, kuna hii barabara inayoelekea Bandarini. Mizigo mikubwa inayoshuka kwenye meli hupitishwa huku.

Hapa ndio njia panda ya Kisosora Na Chumbageni....kushoto unaelekea Deep Sea na hii nyengine inaelekea Horohoro.

No comments:

Post a Comment