BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, August 27, 2010

HUYU NDIO SILIKANTI ALIYEVULIWA TANGA!

Samaki mkubwa wa kihistoria duniani ambaye alikuwa amepotea zaidi ya miaka milioni 65 aliibuka katika Kisiwa cha Nyuli, Pwani ya Tanga na kuvuliwa na wavuvi wa eneo la Sahare Jijini hapa.

Samaki huyo aina ya Silikanti amekuwa akipasua vichwa vya wanasayansi ya viumbe wa majini duniani kutokana na umbile lake kuwa na viwiko vya miguu na mikono, pingili na mafuta mengi tofauti na samaki wengine.

Mshauri wa Uvuvi katika Sekretarieti ya Mkoa wa Tanga, Hassan Juma alitoa taarifa hiyo wakati wa kikao cha waandishi wa habari cha kutambulisha shughuli za mradi wa uhifadhi wa mazingira ya baharini na pwani (MACEMP) kwa Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga.

No comments:

Post a Comment