BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, August 31, 2010

FIVE BROTHERS YATOA MSAADA KWA WATOTO YATIMA

WATOTO wanaolelewa katika Kituo cha kulelea watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu cha Casa delajoa kilichopo chini ya Kanisa Katoliki Jimbo la Tanga wameiomba Jamii kuendelea kutoa misaada ya hali na mali kwa makundi hayo ili waweze kuishi kwa faraja.

Watoto hao wamesema jukumu la kusaidia yatima ni la kila jamii hivyo wanajamii bado wanahitajika Nkushiriki kuwasaidia ili nao waweze kuishi kama watoto wenye wazazi wao.

Mmoja wa watoto hao Monica Eliasi anayalelewa katika kituo hicho ametoa kauli hiyo leo muda mfupi baada ya kupokea msaada wa Vyakula,Sabuni na Maziwa kutoka kwa Kampuni ya Five Brothers Entertainment.

Awali Mkurugenzi wa Kampuni hiyo,Bwana Nassoro Makau ameitaka Jamii Mkoani Tanga kujitoa na kuwasaidia watoto yatima kwani kila mwanajamii anajukumu la kufanya hivyo.

Nae Mlezi wa watoto hao Katika Kituo hicho cha Casa delajoa Sista Josephine Sesf ameishukuru Kampuni hiyo na kutoa wito kwa Jamii kuunga mkono juhudi hizo za kuwasaidia watoto hao kwani hao ni Watoto wa Taifa na ni Watoto wa Mungu.

No comments:

Post a Comment