BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, October 19, 2010

HASSAN SHARIFF AIBUKA MSHINDI WA VODACOM TANGA CYCLING

Mgeni rasmi Bwana Kisheru sambamba na Sophia Wakati akitoa zawadi kwa washindi. Katika mbio hizo za Baiskeli, Hassan Shariff aliibuka kidedea na kuzawadiwa kitita cha Tsh.150,000. Shariff aliupata ushindi huo kwa kuendesha baiskeli ya mwendo yenye umbali wa kilomita 140 yaliyoanzia mkwakwani mpaka hale na kurudi Tanga,kwa kutumia masaa 4.140.01 kwa kuwapita washiriki 26.

Mgeni rasmi katika mashindano hayo Bwana Ndibalema Kisheru akisema neno kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Tanga,Meja Jeneral Said Kalembo, aliishukuru kampuni hiyo ya simu za mikononi Vodacom kwa kudhamini michuano hiyo ya Baiskel mkoani hapa.

Mzee Hiza kiongozi wa waendesha baiskel akitoa maelekezo kwa wandesha baiskel za kawaida maarufu kama 'bodaboda' katika mashindano ya Nyerere Vodacom Tanga Cycling eneo la Mkwakwani mjini Tanga.


Kundi la baiskeli za taili tatu walemavu wakijiandaa kuondoka katika eneo la Mkwakwani

Kundi la baiskeli la matairi mawili, likijiandaa na mashindano hayo.

Kazi ilianza....kila mtu akitaka kuibuka mshindi.

No comments:

Post a Comment