BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, September 24, 2010

WATU WATANO WAKAMATWA NA GONGO KILINDI, TANGA!


Jeshi la polisi la mkoa Tanga linawashikilia watu wa tano kwa kosa la kukutwa lita 110 za pombe haramu ya gongo. Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Liberatusi Sabasi amesema kuwa tukio hilo limetokea Septemba 20 mwaka huu majira ya saa 8 mchana katika Kijiji cha kwekivu wilayani Kilindi.

Sabasi amewataja watuhumiwa hao ni Adamu Aroni miaka 39, Bonge Mwanduro 52, Limbau Ndereko 58 wamekamatwa na lita 110 za gongo , Sila Mondo miaka 24, na Mbalazi Mtuka miaka 52 walikamatwa wakazi wa kijiji cha Kwekivu kitongoji cha Chanungwi wilayani Kilindi.

Kamanda huyo ameendelea kusema watuhumiwa wote ni wafanya biashara na wamefikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

No comments:

Post a Comment