BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Wednesday, September 29, 2010

TAYODEA YATOA SOMO LA UCHAGUZI MKUU 2010!


WANANCHI Mkoani Tanga wamehizwa kuchuja ahadi za wagombea zinazotolewa katika kipindi hiki cha Kampeni ili waweze kuchagua viongozi watakaowaletea maendeleo. Rai hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Vijana na Maendeleo Mkoani Tanga TAYODEA Bwana David Chanyegea wakati akizungumza na Blog hii katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu.

Amesema hatma ya maendeleo kwa Mkoa wa Tanga yako mikononi mwao hivyo ni vema wakapima ahadi za wagombea na kuchagua viongozi bora bila ya shinikizo la mtu au kikundi fulani. Pia amewahimiza wananchi waliojiandikiasha kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura ili kuchagua viongozi wanaowataka.

Na Benedict Kaguo, Tanga.

No comments:

Post a Comment