BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Thursday, September 30, 2010

PROF. MAJI MAREFU AMPA NG'OMBE MAMA SALMA KIKWETE!

MGOMBEA ubunge wa jimbo la Korogwe vijijini Steven Ngonyani Profesa Maji Marefu amempatia zawadi ya ng’ombe mke wa Rais Mama Salma Kikwete kama zawadi ya kuhimiza ufugaji ili kutekeleza Kilimo Kwanza.

Mgombea huyo ubunge ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutokana na kuwa karibu na wananchi na kujishughulisha na kazi za kilimo na ufugaji pamoja na utaalamu wa tiba za asili.

Alisema zawadi hiyo imelenga kumwezesha Mama Salma kufanya kazi ya ufugaji ili kwenda sambamba na kauli mbiu ya Serikali ya Kilimo kwanza kinachosisitiza juu ya kilimo na ufugaji wa kisasa.

Akipokea zawadi hiyo Mke Rais Mama Salma alimshukuru Profesa Maji Marefu kwa zawadi hiyo na kusema kuwa itamsaidia kuongeza zizi lake kwa kufuga ngombe zaidi.

Alisema zawadi hiyo ya ngo’mbe dume itamuwezesha kuongeza ufanisi katika ufugaji wa ngombe ili kujiongezea kipato kupitia ufugaji..

Na Benedict Kaguo, Korogwe.

No comments:

Post a Comment