BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, September 28, 2010

TIMU YA SOKA YA WANAWAKE PONGWE KAMBINI!

TIMU ya soka ya wanawake Pongwe jana imeanza mazoezi yake katika uwanja wa soka Villa kwa ajili ya kujiandaa na michezo mbalimbali ya kirafiki. Akizungumza na Blog hii, Mkurugenzi wa timu hiyo Salim Baawazir amesema kuwa maandalizi ya timu hiyo kwa ajili ya michezo hiyo ya kirafiki yanaendelea vizuri.

Baawazir amesema kuwa timu hiyo itakutana na timu ya Tanga Women Fc katika mchezo ambao unatarajiwa kufanyika Pongwe ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa TRFA Said Sudi.

Ameongeza kuwa timu hiyo inatarajiwa kuelekea wilayani Pangani kwa ajili ya kushiriki michezo mbalimbali ya kirafiki.

Na Oscar Assenga, Pongwe.

No comments:

Post a Comment