BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, September 28, 2010

"MBIO ZA BAISKELI TANGA OCTOKA 14"- SOPHIA WAKATI

(Sophia Wakati, mwandaaji wa mbio za baiskeli Tanga)

MKAKATI wa mashindano ya baiskeli inaendelea kupamba moto jijini hapa baada ya washiriki mbalimbali kujitokeza kuthibitisha kushiriki mashindano hayo ambayo yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi october 14 mwaka huu mkoani hapa.

Akizungumza na Blog hii, mratibu wa michuano hiyo, Sophia Wakati amesema kuwa mpaka sasa tayari ameshaunda kamati ya watu watano wa kujadili mashindano hayo.

(Sophia Wakati akiwa na Oscar Assenga ambaye ni mwandishi wa habari wa gazeti la Bingwa)

wakati amesema kuwa maandalizi ya mashindano hayo yanaendelea vizuri na yamekwisha kamili ambapo kwa sasa wapo katika mkakati wa kutengeneza namba za washiriki ambapo zitakapo kamilika washiriki watakatiwa kupitia vituo mbalimbali vitavyowekwa jijini hapa.

Aidha amesema kuwa namba hizo zitawasaidia washiriki kutambulika katika mashindano hayo ambayo kwa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na msisimuko wa hali ya juu. Watakimbia kilomita 125 Kwa upande wa zawadi mshindi wa kwanza atapata 200,000,wa pili 150,000, wa tatu 100,000,wa nne 75,000 wa tano 50,000.

Mashindano hayo yatawashirikisha walemavu wa viungo ambayo watakimbia kilimeta 5 ambapo mshindi wa kwanza 100,000,mshindi wa pili 75,000,wa tatu 50,000.

No comments:

Post a Comment