BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, September 27, 2010

VODACOM, SOFIA PRODUCTION RAHA TUPU TANGA!



Kampuni ya simu za mkononi Tanzania Vodacom, imefanya jambo la kihistoria mkoani Tanga baada ya kuwapa burudani ya kutosha wakazi wa jijini hapa katika kuadhimisha miaka kumi ya kampuni hiyo kwenye uwanja wa Tangamano.


Shamrasharma hizo zilizoandaliwa na kampuni ya Sofia Production chini ya Aisha Kissoky na kudhaminiwa na Vodacom, pia ziliambatana na burudani kutoka kwa kundi zima la Zanzibar Stars ambao walikonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa Taarab wanaotumia mtandao wa Vodacom. Burudani nyengine ni kutoka kwa Super Baikoko Bazoka, pamoja na vijana wa dansi wa Town Boys.

Umati ukishuhudia kinachoendelea wakati wa miaka kumi ya Vodacom Tanzania kunako uwanja wa Tangamano.

Msema chochote wa kundi la Zanzibar Stars alipkaribishwa kutangaza ratiba ya burudani.

Jumaa Kombo kutoka Sofia Production, akiwa kazini.

Vijana wa Vodacom wakiwa tayari kugawa zawadi kwa watumiaji wa mtandao huo waliokuwa wanajibu maswali ya papo kwa papo yaliyokuwa yanaulizwa uwanjani hapo.

Waimbaji nguli wa muziki wa Taarab nchini kutokea Zanzibar Stars...Jokha Kassim akiwa na mwenzake.

Kundi la Zanzibar Stars likiwa tayari kutoa burudani kwa wapenzi wake waliokuja kufurahi pamoja na kampuni ya Vodacom.

Waimbaji wa Zanzibar Stars wakishuka kwenye gari.

Hii ndio gari iliyowaleta kundi la Zanzibar Stars.

Anaitwa Mwagomero, ndio mwimbaji wa kundi la Super Baikoko Bazoka ya jijini Tanga. Mambo yao sio ya kawaida...ndio wanaongoza kwa Baikoko mkoani hapa!

Mimi (Anko Mo) nikiwa na mama Sofia Production, Aisha Kissoky ndie muandaaji wa shamrashamra hizo zilizodhaminiwa na kampuni ya Vodacom Tanzania.

Huyu jamaa ndio alikuwa analeta raha zote....ni msema chochote wa shughuli nzima. Anaitwa Selemani Mtei.

Mwanadada kutoka kundi la Super Baikoko Bazoka, akifanya mambo yake. Anaiywa Halima.

Haya jamani..Tanga hiyoooo!! Nae kutoka Super Baikoko Bazoka, anaitwa Shakira akifanya mambo yake jukwaani.

Upande wa pili..umati ukishuhudiia mambo ya Vodacom Tanzania

Huduma zote za Vodacom Tanzania zilikuwepo kupitia vibanda hivi. Watu walipata kununua simcard pamoja na vocha zilizokuwa zinauzwa hapo. Hongera sana Vodacom Tanzania, pamoja na kampuni ya Sofia Production kwa kuleta mambo mazuri jijini Tanga.

No comments:

Post a Comment